THOMAS SANKARA (CHE GUEVARA OF AFRICA)

Kapteni:THOMAS SANKARA.
Leo tunawaletea makala ndefu kidogo lakini ni yakusisimua inayo muhusu shuja wa  Burkina Faso  Na Afrika kutokana na sera zake za uongozi huyu ni Kapteni: Noël Isidore Thomas Sankara.
Au wengi walipenda kumuita Che Guevara wa Afika.
VIDEO YA MAISHA YAKE bonya hapa=> https://youtu.be/0SACE0PGUbI
THOMAS SANKARA Alizaliwa munamo tarehe 21 Desemba 1949 mjini YAKO,VOLTA YA JUU. Ambako sasa kuna julikana kama BURKINA FASO. (land of upright men).  Babake, Joseph Sankara, alikuwa Msilimi-Mossi Alijipa jina Ouedraogo alipojiunga na jeshi la UFARANSA wakati wa Vita kuu ya pili ya Dunia. Joseph alikuwa Muislamu, lakini baada ya kujiunga na jeshi, alibadili dini na akawa Mkatoliki. Mamake Sankara alikuwa anaitwa Marguerite Kinda, na alikuwa Mmossi. Baada ya Thomas Sankara kufika ujana, babake aliibadilisha jina ya familia yao tena na wakarudi kuitwa "Sankara". Alipokuwa mdogo, familia yake iliishi mji wa Gaoua, kwani hapo ndipo baba yake alipoajiriwa na jeshi. Shuleni, alifuzu katika masomo ya hisabatiKifaransa na dini. Kwa kuwa alikuwa mchamungu, makasisi wake walimshauri aende shule ya seminari baada ya kumaliza shule ya msingi. Alikubali, lakini pia alifanya mtihani wa kuingia kidato cha sita na kuipita. Babake alipowajulisha makasisi kwamba Sankara hangekuwa anaenda seminari, bali angejiunga na shule ya upili, walimjibu kwa kusema hakumwombea mwanake kwa kina.
Sankara alijiunga na Shule ya Upili ya Ouezzin Coulibaly, iliyokuwa kule Bobo-Dioulasso. Huko, alifanya urafiki na vijana wengi ambao baadaye walikuja kuwa wandani wake alipokuwa serikalini, kama vile Fidele Toe, ambaye akawa waziri, Soumane Toure, nk. Shuleni, aliendelea kuyapenda masomo ya Hesabu na Kifaransa, pamoja na kuanza kuigiza kwenye michezo.
Sankara Akipiga gita
                                                    
Mwaka wa 1966, rais wa kwanza wa Volta ya Juu, Maurice Yameogo, aliondolewa kupitia mapinduzi na kamanda wa jeshi,Sangoulee Lamizana. alichukua uongozi. Lamizana akaanzisha chuo cha wanajeshi mjini Ouagadougou, ambacho kilikuwa cha kwanza nchini. Sankara alisikia kwenye redio tangazo kwamba wanafunzi wa kwanza wa chuo hicho watachaguliwa kutoka waliohitimu shule ya upili. Alipohitimu, alikuwa mmoja wa waliochaguliwa. Wakati huo, alikuwa na umri wa miaka 17.
Baada ya miaka mitatu, alimaliza masomo yake kwenye chuo hicho cha uanajeshi, na kutumwa Antsirabe, nchini Madagascar. kusomea cheo cha uafisaa. Huko, alifundishwa na kujifundisha zaidi ya masomo ya kawaida ya uanajeshi. Masomo ya kilimo, unyunyuzi, na maisha ya raia wa kawaida. Aliyapenda sana masomo yake huko hadi akaomba ruhusa ya kukaa huko kwa mwaka mmoja zaidi.
Sankara alipanda ngazi ya kijeshi hadi cheo cha kapteni Pamoja na mwanajeshi mwenzake Blaise Compaore alishiriki katika chama cha siri cha "maafisa Wakomunisti" waliolenga kupambana na ufisadi uliokuwa ukiendeshwa na watawala..
Mwaka 1981 alikuwa waziri wa mambo ya ndani katika serikali ya kijeshi ya rais Jean-Baptiste Ouédraogo na kupandishwa cheo kuwa waziri mkuu kwa miezi michache kuanzia Februari 1983 Mwezi Mei alikamtawa na kutiwa mbaroni.
 Mapinduzi ya kijeshi yaliyoongozwa na Blaise Compaore yalimfanya kuwa mwenyekiti wa kamati ya mapinduzi na rais wa tano wa Volta ya Juu.
Baada ya mapinduzi kufanikiwa.Sankara alibadilisha jina la nchi kuwa Burkina Faso. Alijulikana hasa kwa amri yake ya kuwa mawaziri na maafisa wote waserikali yake wasitumie magari makubwa bali gari dogo aina ya Renault 5 ambayo ilikuwa gari la bei ya chini iliyopatikana nchini. Burkina Faso
Pamoja na hayo, alishirikisha wanawake wengi katika serikali yake akapiga marufuku tohara kwa wanawake.
Munamo tare 15 0kutoba 1987 Sankara ali uwawa na serikari yake kupinduliwa Mapinduzi ya liyo fanywa na mshilika wake wa karibu ndugu Blaise Compaoré.
ENDELEA KUFUATILIA MAKALA ZETU KUFAHAMU ZAIDI WATU MAARUFU WALIO PITA KATIKA NYAKATI TOFAUTI TOFAUTI
KWAMONI TUANDIKIE
+255758019034.



No comments